Mchezaji wa Benfica anayevutia klabu kuu za Ulaya
MICHEZO
Published on 30/07/2024

Ikiwa klabu yako itakuwekea kipengele cha kuachiliwa cha zaidi ya £100m, kwa kawaida ni ishara kuwa wewe ni mchezaji maalum. Hiyo inaweza kuwa hivyo kwa mchezaji Joao Neves, kiungo wa kati wa Benfica ambaye anatarajiwa kuhamia klabu kubwa msimu huu.

Neves, 19, ameripotiwa kuvutiwa na Manchester United na Arsenal, lakini ni Paris St-Germain ambayo inazungumziwa kuwa klabu anayoelekea kujiunga nayo zaidi.

Kijana huyo tayari ameisaidia klabu yake ya utotoni kutwaa taji la ligi na kucheza michuano ya Uropa kabla ya kufikisha miaka 20.

Je, Neves atafuata nyayo za wachezaji maarufu kama vile Bernardo Silva, Ruben Dias na Enzo Fernandez na kuwa mchezaji anayelekea kujiunga na klabu kubwa kutoka Lisbon?

Neves, mhitimu wa akademi ya klabu ya Benfica, alipata nafasi yake katika kikosi cha kwanza kutokana na kuondoka kwa Fernandez.

Kinda huyo alicheza mechi yake ya kwanza tarehe mosi mwezi Januari 2023 kabla ya Chelsea kutumia kitita kikucha cha fedha kilichovunja rekodi ya Uingereza kumleta kiungo wa kati wa Argentina Fernandez kwenye Ligi ya Premia siku ya mwisho ya uhamisho baadaye mwezi huo.

"Bila Enzo ubora wetu ulipungua," anaelezea Filipe Ingles, kutoka podcast Benfica FM, ambaye alihofia kuwa taji linaweza kupotea kutoka kwa mikono ya Eagles.

Bosi Roger Schmidt alimgeukia Neves miongoni mwa wachezaji wake na kiungo huyo alilipa imani hiyo kwa kufunga bao katika sare ya 2-2 dhidi ya wapinzani wao Sporting ambayo ilionekana kuwa muhimu katika kushinda ligi kwa mara ya kwanza baada ya miaka minne.

"Mchezo uliofuata tulishinda, tulikuwa mabingwa na Joao Neves alikuwa shujaa aliyeokoa siku katika dakika za mwisho," anasema Ingles.

Neves amecheza mechi 50 za Primeira Liga, akianza mara 33 kati ya hizo, huku akifunga mara nne na kusajili moja.

"Alikua kiungo kikuu katika kikosi cha kwanza na pengine alikuwa mchezaji wetu bora msimu mzima," anaongeza Ingles. "Kulikuwa na mechi ambapo meneja na timu alizomewa, lakini sio yeye kamwe. Kwa sababu mashabiki wa Benfica wanamuona kama mmoja wao na huwa anacheza vizuri na kujitolea."

Kiungo huyo pia alifanikiwa kimataifa na hadi sasa ameichezea Ureno mara tisa, ikiwa ni pamoja na katika mechi zao mbili za Euro 2024.

Comments
Comment sent successfully!