soka Ulaya
HABARI
Published on 23/07/2024

Manchester City wanatafuta kumnunua winga wa Crystal Palace Eberechi Eze, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 26 akiwa na kipengele cha kuachiliwa cha £60m pamoja na nyongeza. (Mirror),

Klabu ya Saudi Arabia Al-Ittihad inamtaka mchezaji wa Ubelgiji Kevin de Bruyne, 33, jambo ambalo limepelekea Manchester City kufikiria kumnunua Eze. (Guradian)

Manchester City wanavutiwa na mlinda mlango wa Paris St-Germain na Italia Gianluigi Donnarumma, 25, huku wakitafuta kuchukua nafasi ya Ederson mwenye umri wa miaka 30 wa kimataifa wa Brazil, ambaye anaweza kuhamia Al-Ittihad. (Sky Sports Italia)

Ederson atagharimu angalau pauni milioni 40 ikiwa Al-Ittihad wanataka kumsajili kutoka Manchester City, ambao wako tayari kumwacha kipa huyo aondoke mradi tu hesabu yao ifikiwe. (ESPN)

Tottenham inamthamini mshambuliaji wa Brazil Richarlison kwa pauni milioni 60, huku klabu ya Saudi Pro League Al-Ahli ikionyesha kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Times – Subscription Required)

PSG inamtaka winga wa Manchester United Jadon Sancho, 24, na mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza anaonekana kuwa tayari kwa wazo la kujiunga na mabingwa hao wa Ufaransa. (foot Mercato – In French)

PSG watajaribu kufanya makubaliano na Manchester United kumnunua Sancho lakini pia wanamtaka kiungo wa kati wa klabu hiyo ya Old Trafford na Ureno Bruno Fernandes, 29. (L'Equipe – In French),

Aston Villa wanalenga kumnunua fowadi wa Atletico Madrid na Ureno Joao Felix, 24, baada ya kukubali kuuzwa kwa winga Mfaransa Moussa Diaby, 25, kwa Al-Ittihad kwa £50m. (Guardian)

Winga wa Spurs Bryan Gil, 23, na beki wa kushoto mwenye umri wa miaka 27 Sergio Reguilon, ambao wote ni Wahispania, wameachwa katika ziara ya kujiandaa na msimu mpya wa klabu hiyo nchini Japan na Korea Kusini ili waweze kutafuta uhamisho kutoka kwa klabu hiyo. (Standard)

Newcastle United wamefanya mazungumzo na meneja Eddie Howe ili kumhakikishia juu ya upeo wa jukumu lake, na klabu hiyo ina imani kuwa ingekataa kuchukua nafasi ya kocha wa England ikiwa kuna nia ya Chama cha Soka. (Telegraph – Subscription Required)

Arsenal wako tayari kumpa mshambuliaji wa Uingereza Eddie Nketiah, 25, kama sehemu ya makubaliano ya kubadilishana na Crystal Palace kumnunua beki wa Uingereza Marc Guehi, 24. (Metro),

Manchester United na West Ham wako kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa kulia wa Morocco, Noussair Mazraoui kutoka Bayern Munich, ambaye wanataka takriban pauni milioni 19 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Sky Sports in Germany),

West Ham wanaweza kutafuta dili la kumnunua beki wa kulia wa Manchester United Mwingereza Aaron Wan-Bissaka mwenye umri wa miaka 26 ikiwa Mazraoui atahamia Old Trafford. (Sky Sports),

Mazungumzo kati ya Paris St-Germain na Napoli kuhusu mkataba wa kumnunua mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 25, yamekwama. (Fabrizio Romano),

Besiktas wamemwambia kiungo wa kati wa zamani wa Arsenal, Liverpool na England Alex Oxlade-Chamberlain, 30, kwamba hayupo tena katika mipango yao. (Mirror)

Comments
Comment sent successfully!